close
Nenda kwa yaliyomo

Ulaya

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Ulaya (asili ya jina ni neno la Kiarabu ولاية, wilaayatun[1]; inaitwa pia Uropa kutoka Kigiriki: "Ευρώπη", jina la mungu jike Europa) ni bara lililoko katika Kaskazini ya Dunia, likipakana na Bahari ya Aktiki upande wa kaskazini, Bahari ya Atlantiki upande wa magharibi, na Bahari ya Mediterania upande wa kusini. Mpaka wake wa mashariki kwa kawaida hufafanuliwa kupitia Milima ya Ural, Mto Ural, Bahari ya Kaspi, Milima ya Kaukazi, na Bahari Nyeusi, ingawa mipaka hii ni ya kijiografia na kihistoria zaidi kuliko ya kisiasa. Kwa eneo la takriban kilomita za mraba milioni 10.18, Ulaya ni bara dogo la pili baada ya Australia lakini lina idadi kubwa ya watu, ikifikia zaidi ya milioni 750, na hivyo kuwa moja ya maeneo yenye msongamano mkubwa wa watu duniani.

Ulaya ina historia ndefu na imechangia pakubwa katika maendeleo ya kisiasa, kiuchumi, na kitamaduni duniani. Bara hili lina mataifa 44 yanayotambulika kimataifa, yakiwemo mataifa makubwa kama Ujerumani, Ufaransa, na Uingereza, pamoja na madola madogo kama Vatikani na Liechtenstein. Umoja wa Ulaya (EU) ni moja ya miungano muhimu ya kisiasa na kiuchumi katika bara hili, ukiwa na wanachama 27. Aidha, Ulaya imekuwa kitovu cha mapinduzi mbalimbali, kuanzia Mapinduzi ya Kitaaluma na ya Viwanda hadi maendeleo ya demokrasia ya kisasa, na imeendelea kuwa na ushawishi mkubwa katika masuala ya kimataifa.

Ramani

BERJAYA
Ulaya kutoka angani.
BERJAYA
Ulaya duniani.
BERJAYA
Lugha za Ulaya.
BERJAYA
Kanda za kiutamaduni za Ulaya kadiri ya Ständiger Ausschuss für geographische Namen (StAGN) ya Ujerumani.
BERJAYA
Ulaya mwaka 1000 hivi.

Utawala

Katika karne ya 20, baada ya vita kuu mbili, nchi mbalimbali za Ulaya zilianza kushirikiana kwa njia mbalimbali:

Kanda za Ulaya

Katika orodha inayofuata kanda zinatajwa katika utaratibu wa Umoja wa Mataifa (UN categorisations/map). Lakini utaratibu huo haukubaliki ndani ya Ulaya kwa nchi za Ulaya ya Kati. Wajerumani, Waaustria, Waswisi, Wacheki, Waslovakia na Wapolandi hukubaliana ya kwamba wenyewe si Ulaya ya Magharibi wala ya Mashariki ila Ulaya ya Kati. Kuna majadiliano kuhusu mipaka ya kanda hili yasiyokwisha bado, kwa mfano suala la Hungaria au Latvia.

Ulaya Mashariki

NchiBenderaMji MkuuIdadi ya Watu (2024)
BelarusBERJAYAMinsk9,200,000
BulgariaBERJAYASofia6,400,000
Jamhuri ya CzechBERJAYAPrague10,500,000
HungaryBERJAYABudapest9,600,000
MoldovaBERJAYAChisinau2,500,000
PolandBERJAYAWarsaw37,700,000
RomaniaBERJAYABucharest19,000,000
RussiaBERJAYAMoscow144,000,000
SlovakiaBERJAYABratislava5,400,000
UkraineBERJAYAKyiv36,000,000

Ulaya ya Kaskazini

NchiBenderaMji MkuuIdadi ya Watu (2024)
DenmarkBERJAYACopenhagen5,900,000
EstoniaBERJAYATallinn1,300,000
FinlandBERJAYAHelsinki5,600,000
IcelandBERJAYAReykjavik380,000
IrelandBERJAYADublin5,100,000
LatviaBERJAYARiga1,800,000
LithuaniaBERJAYAVilnius2,700,000
NorwayBERJAYAOslo5,500,000
SwedenBERJAYAStockholm10,500,000
UingerezaBERJAYALondon68,000,000

Ulaya ya Magharibi

NchiBenderaMji MkuuIdadi ya Watu (2024)
AustriaBERJAYAVienna9,100,000
UbelgijiBERJAYABrussels11,800,000
UfaransaBERJAYAParis65,000,000
UjerumaniBERJAYABerlin83,000,000
LiechtensteinBERJAYAVaduz39,000
LuxembourgBERJAYALuxembourg (jiji)660,000
MonacoBERJAYAMonaco (jiji)39,000
UholanziBERJAYAAmsterdam17,800,000
UswisiBERJAYABern8,800,000

Ulaya ya Kusini

NchiBenderaMji MkuuIdadi ya Watu (2024)
AlbaniaBERJAYATirana2,800,000
AndorraBERJAYAAndorra la Vella79,000
Bosnia na HerzegovinaBERJAYASarajevo3,200,000
KroatiaBERJAYAZagreb3,800,000
CyprusBERJAYANicosia1,200,000
UgirikiBERJAYAAthens10,200,000
ItaliaBERJAYARome59,000,000
MaltaBERJAYAValletta520,000
MontenegroBERJAYAPodgorica620,000
Macedonia KaskaziniBERJAYASkopje1,800,000
San MarinoBERJAYASan Marino (mji)34,000
SerbiaBERJAYABelgrade6,600,000
SloveniaBERJAYALjubljana2,100,000
HispaniaBERJAYAMadrid47,800,000
Vatican CityBERJAYAVatican City (mji)800
UrenoBERJAYALisbon10,100,000

Nchi za Ulaya

Orodha kamili ya nchi za Ulaya ikitaja ukubwa wa eneo, idadi ya watu, miji mikuu na miji mikubwa zaidi pamoja na lugha rasmi. Orodha hii haionyeshi ukanda wa nchi husika. Tazama juu kupata kanda za Ulaya.

Orodha ya Nchi na Maeneo ya Ulaya
BenderaNchi/MaeneoEneo (km²)Idadi ya WatuMji MkuuJiji KubwaLugha Rasmi
BERJAYAAlbania28,7482,829,741TiranaTiranaKialbania
BERJAYAAndorra46879,034Andorra la VellaAndorra la VellaKihispania
BERJAYAArmenia29,7432,767,923YerevanYerevanKiarmenia
BERJAYAAustria83,8799,006,398ViennaViennaKijerumani
BERJAYAAzebajani (zaidi ni Asia)86,60010,353,269BakuBakuKiazabajani
BERJAYAAislandi103,000366,425ReykjavikReykjavikKiaislandi
BERJAYAAyalandi70,2734,994,724DublinDublinKiingereza, Kigaeli
BERJAYABelarusi207,6009,349,645MinskMinskKibelarusi, Kirusi
BERJAYABulgaria110,9936,447,710SofiaSofiaKibulgaria
BERJAYABosnia na Herzegovina51,1973,276,000SarajevoSarajevoKiserbia, Kikroeshia, Kibosnia
BERJAYAEstonia45,2271,331,796TallinnTallinnKiestonia
BERJAYAHungaria93,0289,606,259BudapestBudapestKihungaria
BERJAYAItalia301,34060,317,116RomeRomeKiitalia
BERJAYAJojia (zaidi ni Asia)69,7003,688,600TbilisiTbilisiKijojia
BERJAYAKorasia56,5943,850,695ZagrebZagrebKikorasia
BERJAYAKosovo10,8871,798,188PristinaPristinaKikosovo
BERJAYAKupro9,2511,244,188NicosiaNicosiaKigiriki, Kituruki
BERJAYALatvia64,5891,882,000RigaRigaKilatvia
BERJAYALiechtenstein16039,315VaduzSchaanKijerumani
BERJAYALithuania65,3002,794,000VilniusVilniusKilithuania
BERJAYALuxembourg2,586634,814Luxembourg CityLuxembourg CityKifaransa, Kijerumani, Kiluxembourg
BERJAYAMalta316514,564VallettaBirkirkaraKimalta, Kiingereza
BERJAYAMoldova33,8462,603,000ChisinauChisinauKimoldova
BERJAYAMonako2.0239,511MonacoMonacoKifaransa
BERJAYANorwei385,2075,391,369OsloOsloKinorwei
BERJAYAPolandi312,69638,265,017WarsawWarsawKipolandi
BERJAYASan Marino6133,600San MarinoSan MarinoKiitalia
BERJAYAUbelgiji30,68911,584,008BrusselsAntwerpKiholanzi, Kifaransa, Kijerumani
BERJAYAUcheki78,86610,686,269PraguePragueKicheki
BERJAYAUdeni42,9255,932,654CopenhagenCopenhagenKideni
BERJAYAUfaransa551,69568,042,591ParisParisKifaransa
BERJAYAUfini338,4245,541,037HelsinkiHelsinkiKifini, Kiswidi
BERJAYAUfalme wa Muungano243,61067,736,802LondonLondonKiingereza
BERJAYAUgiriki131,95710,724,599AthensAthensKigiriki
BERJAYAUhispania505,99047,450,795MadridMadridKihispania
BERJAYAUholanzi41,54317,407,585AmsterdamRotterdamKiholanzi
BERJAYAUjerumani357,02283,190,556BerlinBerlinKijerumani
BERJAYAUreno92,09010,295,909LisbonLisbonKireno
BERJAYAUrusi (Sehemu ya Ulaya)17,098,242146,599,183MoscowMoscowKirusi
BERJAYAVatikani0.49825Vatican CityVatican CityKilatini, Kiitalia

Tanbihi

1. Kanda zinazotajwa (Ulaya ya Kusini – magharibi n.k.) zinafuata utaratibu wa Umoja wa Mataifa UN categorisations/map. Nchi kadhaa zinazotajwa hapo chini zinaweza kuhesabiwa kuwa sehemu ya Ulaya na pia bara nyingine (Asia, Afrika, au Oceania). Hii inategemea na namna ya kugawa kontinenti; pia wakazi wenyewe wanaweza kujielewa tofauti na majirani yao.

2. Urusi ni nchi ya kontinenti mbili za Ulaya ya Mashariki na Asia; namba za wakazi na za eneo zimetasjwa kwa ajili ya sehemu ya Kiulaya pekee.

3–5. Guernsey, Kisiwa cha Man, and Jersey ni maeneo ya kujitegemea chini ya Taji la Ufalme wa Uingereza.

6. Namba za Ureno hazijumlishi Visiwa vya Madeira, ambazo ni sehemu ya Ureno magharibi ya Marokko katika Afrika.

7. Namba za Hispania hazijumlishi Visiwa vya Kanari magharibi ya Marokko katika Afrika, wa maeneo ya Ceuta na Melilla ambayo ni sehemu za Hispania kwenye pwani ya Moroko, Afrika ya Kaskazini.

8. Namba za Ufaransa hazijumlishi maeneo yake yaliyopo Amerika ya Kati au Kusini, Bahari Hindi au Oceania.

9. Uholanzi: Idadi ya wakazi ni ya 2004; Amsterdam ni Mji Mkuu lakini Den Haag ni makao makuuy a serikali.

10. Armenia huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki

11. Azerbaijan huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee.

12. Kupro huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Kusini; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu zisozo chini ya Dola ya Kituruki ya Cyprus.

13. Georgia huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee.

14. Uturuki ni nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Kusini; namba zinazotajwa zinahusiana na sehemu ndogo ya Magharibi pakee iliyomo Ulaya hasa jimbo lote la Istanbul.

15. Kazakhstan huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee.

Tazama pia

Marejeo

  1. Hivyo asili ya neno "Ulaya" ni sawa na "wilaya"; Krapf 1882 Swahili-English dictionary anaeleza: ""ULAYA (WALAYA au WILAYA ya) ... mother-country in contradistinction to colonies, foreign possessions or parts"; Sacleux 1939 Dictionnaire Swahili-Francais anataja kama etimolojia ya Ulaya "Ar. Hind. ولاية wilaya, pays etranger" (=nchi ya kigeni); Madan 1903 "Wilaya, n. (1) native land, home, but commonly used of foreigners, and so (2) Europe. Ulaya Uzungu, Europe. U, Hindi, India. Ulaya wa Wareno, Portugal